Ukuaji wa Kiafrika ni harakati, sio ubabaishaji, anasema mchumi na aliyekuwa Waziri wa Fedha wa Nigeria Ngozi Okonjo-Iweala. Katika mazungumzo haya ya kusisimua yaliyo wazi,Okonjo Iweala anaelezea hatua endelevu barani na kuainia changamoto nane ambazo mataifa ya Kiafrika bado yanahitaji kuzungumzia ili kuweza kuwa na maisha bora baadaye.
