Maisha ya Memory Banda yalichukua njia ya tofauti na maisha ya dada yake. Dada yake alipovunja ungo, alipelekwa katika kambi ya awali ambayo inafundisha wasichana "jinsi ya kumridhisha mwanaume kimapenzi" Akapata uja uzito huko - akiwa na umri wa miaka 11. Lakini Banda akakataa kwenda. Badala yake , akaandaa wengine na akamuomba kiongozi wa jamii yake kupitisha sheria ndogo inayozuia wasichana kulazimishwa kuolewa kabla ya kufikisha miaka 18. Akaendeleza mapambano haya mpaka katika ngazi ya kitaifa ... akipata matokeo ya ajabu sana kwa wasichana wote , katika nchi yote ya Malawi.
