Watu millioni sitini na tano walitolewa katika makazi yao na migogoro na majanga katika mwaka 2016. Huu sio tu ni mgogoro; lakini pia ni kipimo cha kuwa sisi ni nani na tunasimamia nini, anasema David Miliband - kila moja wetu ana jukumu binafsi kutatua hali hii. Katika mazungumzo haya yenye umuhimu wa kipekee kuyaangalia , Miliband anatupa njia za dhahiri za kuwasaidia wakimbizi na kugeuza huruma na kuwawazia wengine kuwa vitendo.
